Hatimaye Pedro Rodriguez amechukua uamuzi huu kuhusu uhamisho wake.
Pedro mwenye asili ya visiwa vya
Canary, amekuwa akihusishwa na kujiunga na Manchester United, na usiku
wa leo kocha Luis Enrique alimuweka benchi huku mkurugenzi wa michezo wa
timu hiyo Robert Fernandez amekiambia kituo cha Esport 3 kwamba Pedro
ameomba kuhama.
“Pedro amenitaarifu rasmi kwamba
anataka kuondoka, ila kwa sasa bado hatujapata ofa. Ikiwa kuna klabu
inayomtaka basi itabidi walipe fedha ya kuweza kuvunja mkataba wake
ambayo ni £21m.”

Klabu
ya Manchester United inaripotiwa kuwa kwenye mazungumzo ya kina na
Barcelona na muda wowote kutoka sasa inatarajiwa wataafikiana juu ya
uhamisho huo.
No comments:
Post a Comment